Bima Nafuu ya Afya

Habari za Kitaifa (source Habari Leo)Makabwela kunufaika na bima nafuu ya afya
Imeandikwa na Namsembaeli Mduma; Tarehe: 6th December 2010 @ 23:40  visits http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=12295

  
 
 
 
 

 
 

WATANZANIA wa kipato cha chini wataanza kunufaika na bima mpya ya afya ya bei nafuu kutoka kwa Wakala wa Kwanza wa Bima Ndogo itakayoanza kutolewa kwa majaribio Dar es Salaam hivi karibuni, ili kuwaondoa katika hatari ya kupoteza maisha kwa maradhi, kutokana na kipato duni chao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa bima hiyo Dar es Salaam jana, Meneja Mradi wa wakala huo, Wilson Mnzava alisema sambamba na bima hiyo ya afya, Watanzania hao watanufaika na bima nyingine ya Kilimo Kwanza na ile ya mikopo itakayowafanya warejee katika hali zao za kawaida, baada ya kupata matatizo yatakayosababisha washindwe kurejesha mikopo watakayokuwa wamekopa kutoka

kwa wakopeshaji wao.

Mnzava alisema bima hiyo ya afya inalenga kuiunga mkono Serikali katika vita yake

dhidi ya maradhi na vifo vinavyosababishwa na hali duni ya kipato cha mwananchi

inayomfanya ashindwe kumudu gharama za matibabu.

Alisema wakala wao anahudumia Watanzania watakaokuwa

wamejiunga kwenye vikundi vya watu wasiopungua watatu

ambao watakuwa wanajihusisha na vikundi vya uzalishaji kama vile Saccos,

benki au vingine vya biashara.

Alisema gharama watakayotozwa kwa mwezi ni Sh 3,500 hadi 4,000 tu na kwamba

watakuwa na haki ya kuuelekeza wakala endapo wanataka kulipiwa

matibabu hospitalini au kulipwa fedha.

Katika hilo bima hiyo na nyingine ya afya, alisema kwa siku saba

atakazokuwa amelazwa mteja wao na kuamua familia yake ilipwe, bila kujali

atakaa hospitali kwa muda gani, atalipwa Sh 10,000 kila siku kwa siku saba,

na hiyo itafanywa kwa kila mwana familia yakeatakayeugua.

Huduma nyingine ya bima iliyozinduliwa ni ile ya Kilimo Kwanza

ambapo mwananchi mwenye mazao yatakayokuwa yameathiriwa na janga lolote,

 atalipiwa gharama alizokopa kwa ajili ya kilimo hicho.

Kadhalika, kwa wale wenye mikopo katika asasi au benki mbalimbali

nao watalipiwa mikopo yao pale watakapokuwa wamepata vilema vya maisha au

kupoteza maisha, au sababu zingine zitakazowafanya washindwe kuendelea

 kulipa mikopo hiyo. “Hii ni faida kwa Watanzania, tumeanza kufanya hivyo

kwa benki ya wanawake miaka miwili iliyopita, tumewekea bima mikopo ya

wanavikundi wao waliojiunga nasi,” alieleza Mnzava.

wwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwwww

afya njema launch

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out / Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out / Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out / Change )

Connecting to %s


Follow

Get every new post delivered to your Inbox.